''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, April 14, 2019

UPENDO

Mhubiri: Mch. Kiongozi Abdiel M. Mhini 
Maandiko: Yohana 3 :16-17

Yohana 3:16-17 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye."

Yohana 13:34 "Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo."

Yohana 15:12-14  "Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi. Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.  Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo."

Ni jinsi gani Upendo wa Mungu uliyo mkuu kwetu. Aliamua kumtoa mwana wake wa pekee ili tukombolewe. Wiki hii tunakumbuka kifo cha Yesu, jinsi alivyotoa maisha yake kwa ajili yetu. Upendo huu ni mkuu sana. 

Na sisi Yesu alituachia amri kuu, kwamba tupendane sisi kwa sisi, tuwapende maadui zetu. Je ni kwa kiasi gani umempenda jirani yako?, je ni kwa kiasi gani unampenda adui yako?

No comments:

Post a Comment