''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, March 3, 2013


UJUMBE WA LEO: KUMJUA YESU KIBINAFSI
 ------------------------------------------------------
MAANDIKO YA SOMO: Mathayo 16:13-20
MHUBIRI: Mch. MUSSA ELIAS
-----------------------------------------------
Yesu aliwauliza wanafunzi wake “Watu hunena Mwana wa Adam kuwa ni nani?”, Simon Petro alijibu Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu alite hai. Je? Kwendana na maisha yako, Yesu ni nani kwako?. Yesu ni mwamba kwahiyo akikaa kwako na weweukikaa ndani yake, utakuwa imara hata ukipita katika majaribu magumu hutatetereka. Ili uishi maisha  mazuri ni lazima ujenge nyumba yako kwenye mwamba

Ukimjua Yesu kibinafsi hutatishwa na malango ya kizimu. Unaweza kiuwa unatembea na Yesu lakini usimjue kibinafsi. Wanafunzi wa Yesu walikaa na Yesu kwa miaka 3 lakini sio wote waliomfahamu Yesu au kumuelewa vizuri, Yesu aliposema nitasulubishwa Petro akamwambia hutakufa lakini Yesu akasema rudi nyuma wewe shetani. Petro kwa wakati ule hakujua malengo ya Yesu ni nini, hakumfahamu Yesu kibinafsi. Pia Yesu aliwaambia wanafunzi wake siku ya 3 yaani ya ufufuo kwamba atakuwepo Galilaya lakini cha kushangaza siku ya 3 ilipofika wakaenda kumwangalia kaburini. Inaonyesha kuwa walikaa na Yesu kwa muda mwingi lakini hawakuamini alichowaambia.

Hii inamaanisha kwamba unaweza ukawa umeokoka vizuri tena una muda mrefu katika wokovu lakini usiwe unamjua Yesu kibinafsi kwasababu husomi Neno la Mungu pia huombi. Unahitaji kusoma Neno la Mungu ili umjue Yesu kibinafsi, usisubiri kuja kulisoma kanisani.   


No comments:

Post a Comment