''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, January 19, 2014

MALENGO KWENYE MAONO ULIYONAYO

MHUBIRI: MR. OKECH
SOMO:  Kutoka 4:2, Kutoka 14:13

Je,  ukiwa na maono ya mwaka huu ni nini hasa ungependa kutekeleza?, Leo chukua muda  andika kwenye daftari  mambo yote unayotaka kutimiza katika mwaka huu na uandike gharama zake.    

MALENGO KATIKA ELIMU
 Ili maono yako yatimie unahitaji elimu kwahiyo ni vema uweke malengo utakavyojielimisha wewe, watoto wako, ndugu zako.  Elimu ni kitu cha lazima, haijalishi ni elimu gani, kune elimu ya kuipatia shuleni lakini pia kuna ile ya  kujifunza kutoka kwa watu. 

MALENGO KATIKA BIASHARA NA KAZI
Uzembe na Uvivu ni adui mkubwa sana wa maendeleo. Mambo ya uzembe na uvivu yasitajwe tena kwenye maisha yako, na kuna watu hawana cheti chochote na hawana kazi lakini usijikie kwamba Mungu amekusahau Mungu anajua hilo, ni jukumu lako wewe kuweka mambo yako sawa.  Musa aliulizwa na Mungu una nini mkononi na akatumia fimbo hiyo hiyo kuokoka wana wa Israel.
 Pia kwa wafanyakazi ni muhimu sana kufungua biashara yako ya binafsi LAKINI chagua biashara ambayo haitakuwa na muingiliano kwenye kazi zako ili kuepusha majaribu, biashara yako isipunguze ufanyaji kazi wako kazini.  Ukiamua kufanya  biashara kuwa nayo “serious”.  

Kila mtu amepewa karama na huduma yake, Mungu amekupa kitu cha kufanya, Amua kitu ulichopewa kufanya kwa bidii, hata kama una kazi yaaani upo kazini, usisubiri mpaka jumapil fanya kazi ya Mungu muda wowote unaoupata.
Pia katika familia ni muhimu sana wana ndoa kuamabiana malengo yao,. MTAZAMO WAKO KATIKA MAISHA HAYA YANAWEZA KUFANYA UFIKE AU USIFIKE KATIKA MAONO YAKO,  inategemea unaona maisha yako yapoje, unapotazama maisha yako, kile Mungu alichokupa katika maisha yako, ukijiona kama panzi mbele ya majitu utabaki kuwa panzi hivyo hivyo lakini ukiwa na mtazamo wa joshua na kalebu wa kuwaona majitu si kitu utashinda, haijalishi upo katika hali gani au una masiha gani lakini inategemea wewe unajiona kama nani, kama mwanafunzi ukijiona wewe ni mtu wa kufeli utaendelea kufeli lakini ukijiona ni mtu wa kufaulu utafaulu tu.

Mr. Okech akiwa anahubiri

Mr. Okech akiwa anahubiri

Watu wakiombewa Mungu awafanikishe kutimiza maono yao

Familia ya Zayumba ikimshukuru Mungu kwa kuwaponya na ajali ya moto

No comments:

Post a Comment