''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, May 25, 2014

IBADA YA LEO



YATUPASA KUWA NA UKIRI WA WAZI MBELE YA MATAIFA

Kwa  kuwa wokovu wa Yesu Kristo ni njia kuu ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni, kwa kila anayeliamini Jina la Yesu, habari zake zitanenwa kwa mataifa yote kwa ujasiri wote. Kwa kuwa anayekusudia kunena habari za Yesu, anao ushuhuda juu ya Yesu Kristo; huwa ni shahidi ambaye anasimamia kweli yote. Mtume Paulo alikuwa na ujasiri wote wa kumkiri Yesu mbele za mfalme Agripa.

Maelezo ya msingi ya Paulo mbele za mfalme Agripa ni ushuhuda wa kuitwa kwake na Yesu Kristo, kwa jinsi ambayo alitokewa adhuhuri ile akiwa anatekeleza agizo la Wakuu wa makuhani kwenda Dameski kuwapeleka na kuwatesa watakatifu walioliamini jina la Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao. (Mdo 26: 1-32). Naye mfalme Agripa alikuwa tayari kusikiliza ushuhuda wa Paulo. Paulo akasema “Kwa hiyo Ee mfalme Agripa sikuyaasi yale maono ya mbinguni, bali kwanza niliwahubiri wale wa Dameski na Yerusalemu na katika nchi yote ya Uyahudi na watu wa Mataifa kwamba watubu na kumwelekea Mungu wa kuyatenda matendo yanayopatana na kutubu kwao”. (Mdo 26: 12-20).

Vitisho vya mfalme Agripa kwamba usomi wake umempa wazimu wa kumgeuza akili. (Mdo 26: 24). Jibu la Paulo ni la ujasiri kwamba “Sina wazimu Ee Festo mtukufu bali nanena maneno ya kweli na ya akili kamili” (Mdo 26: 25). Agripa kwa hoja yenye nguvu ya Paulo anakwepa ukweli huo ambao ungemgeuza kumpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wake. Kuchomwa moyo kwa mfalme Agripa kulimpa ukweli kwamba Wokovu u-katika Yesu Kristo pekee. Agripa hakuona kosa kwa Paulo, ambalo lingempasa apelekwe mbele kwa Kaisari.

Tunajifunza kwamba vitisho vya mtawala wa ulimwengu ambaye ndiye shetani havitakoma. Imewapasa waamini kumtangaza Yesu Kristo kwa ujasiri wote katika mapito mbalimbali magumu. Paulo aliingia Rumi na kuhubiri huko.
Ingewezekana kabisa kwa Paulo kukubali desturi za Kiyahudi, kwani alikuwa ni Farisayo. Lakini alisimamia kweli ya Yesu Kristo aliyemwokoa, na kumwagiza kuwaendea mataifa. Paulo alikaa kufungoni miaka miwili – aliutumia muda huo kuandika vitabu – Waefeso, Wafilipi, Wakolosai, na Filemoni mnamo 63 BK. Baadaye aliachiliwa huru. Na baadaye aliandika ITimotheo, na Tito, na kifungo cha pili aliandika 2Timotheo. Aliuwawa 67 BK.

No comments:

Post a Comment