''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, June 23, 2019

UMUHIMU WA NENO LA MUNGU

Mhubiri: Dr. Elifuraha Mumghamba
Maandiko: Mathayo 3:13-17, 4:1-11, Kutoka 8:2-3

Mstari wa kukumbuka
Mathayo 4:3-4 "Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu."

Mtu hataishi kwa mkate tu, maisha yako hayapo katika vitu ya kushikika bali yapo katika kila Neno litokalo katika kinywa cha Mungu. Yesu alisema hayo baada ya kujaribiwa na shetani alipokuwa katika mfungo wa siku 40.

Uhai wako uko katika Neno la Mungu, uhai wako hauko katika chakula pekee. Neno la Mungu ni la muhimu sana kwako. Uhai wetu uko katika Yesu mwenyewe.

1Wakorintho 10:1-6 "Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; 2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; 3 wote wakala chakula kile kile cha roho; 4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. 5 Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. 6 Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani."

Wana wa Israel walikula mana njiani lakini walifia njiani, kwasababu walimkasirisha Mungu, na hayo yaliandikwa ili na sisi tujifunze. Neno la Mungu liwe ni namba moja kwako. Ni hatari sana kutegemea vitu vya hapa duniani au kumtegemea mtu.




No comments:

Post a Comment