''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, December 22, 2013

NEEMA YA UTOAJI

MHUBIRI: Mch. Abdiel Mhini
Maandiko: 2Wakoritho 8:6-10

Kuna neema ya utoaji, kuna baraka nyingi katika utoaji, kwanini kutoa sio hiari bali ni lazima kutoa, kila kitu ulichonacho ni cha Mungu na ni Bwana amekupa. Kutoa 
ni amri sio hiari. Unaweza kutumia mali zako kwa faida ya Bwana, kila kiu ni cha Bwana ndomana Kila siku asubuhi inabidi umshukuru Mungu hata kwa hewa ya kutosha. 

Mungu alitoa akatupa vyote tulivyonavyo sasa ni zamu yetu sasa kutoa kwa Bwana aliyetupa tulivyo kuwa navyo. Munggu ndiye mkuu sana na ndiye muumbaji wa mbingu na daniel,

 1Mambo ya nyakati 16:29, unapokuja nyumbani mwa Mungu unatakiwa uje na sadaka yako, unapoichukua sadaka yako unaangalia ukuu wa bwana, kutoa ni chanzo cha baraka, kuna watu wanaokuja nyumbani mwa Bwana mikono mitupu. Sasa tunatoaje kwa bwana? hilo ni swali la kujiuliza mwenyewe. Unapoona Mungu amekutendea ni vizuri kumshukru 

 1 Korithno 16:1-2, toa kiwango kinacholinga, alafu utaona baraka nyingi?. Ni mara ngapi umetoa kulingana na kiasi Mungu alichokufanikisha, hatua zaidi katika Utakatifu wetu, piga hatua na utoe kwa hiari 

1Mambo ya nyakati 29:9, Unapotoa kwa furaha.Unapotoa, Mungu anaona moyo wako, Mungu Anaangalia moyo wa mtoaji. Mathaayo 6:20-21, hautoi kwasaababu kwaajili ya mchungaji, Bwana wetu anarudi upese, kuwa mtoje nao.  

KWA JINSI ULIVYOTOA MWAKA 2013 MWAKA UNAOKUJA PIA HATUA ZAIDI, MUNGU AMEKULINDA MENGI MWAKA HUU NA UKO MZIMA WA AFYA, HUU NI WAKATI WAKO SASA KUSEMA ASANTE KWA BWANA, MWAMBIE BWANA NAOMBA HATUA ZAIDI KWA HABARI KUTOA KWANGU. TAMBUA KWAMBA KUNA NEEMA YA UTOAJI.

1 comment:

  1. Kutoa sio chanzo Cha Baraka-Chanzo Cha BARAKA ni KAZI aliyoifanya KRISTO MSALABANI

    ReplyDelete