''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, November 29, 2015

KUMWAMINI MUNGU

Mhubiri: Mr. Kinabo
Maandiko: 1Wafalme 17:5-16

MUNGU alimchagua Elia kwa kwasababu Elia alichukua hatua ya ki-imani juu ya Mungu anayemwamini. Hivyo nasi pia kama watu wa Kristo yatupasa kuchukua hatua ya ki-imani. Mungu hufanya kitu kwa mtu ambaye anachukua hatua ya kiimani katika kumtumikia Yeye kwahiyo Elia alichukua hatua ya kufanya kitu katika imani.
 
Mungu ana njia nyingi za kufanya vitu kwa watu wake,ina maana kwamba Mungu anapofanya vitu kwa watu wake, hafanyi vitu vyote katika njia moja bali kila mtu kwa njia tofauti.
 
kila mtu kati yetu inampasa kumwamini Mungu na kitu cha muhimu katika kumwamini Mungu yakupasa wewe peke yako bila kumtegemea mwanadamu upige hatua ya ki-imani huku ukiamini kuwa Mungu atafanya kwa wakati wake,yatupasa kumwamini Mungu ili kupiga hatua sawasawa na makusudi ya mungu.

1.  Unapomwamini Mungu ni lazima uchukue hatua

2.  Ni bora kutoa kuliko kupokea.
3. Kutokuwa na woga 1 wafalme 17:13a ki-imani kumuonyesha Mungu kuwa unamwamini kuliko chochote ili naye akapate kufanya kazi na wewe sawasawa na mapenzi yake.

 

No comments:

Post a Comment