''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, February 16, 2014

JUKUMU LA UMISHENI KWA KANISA LA MAHALI PAMOJA

MHUBIRI: Mch. Kiongozi Mhini
Maandiko: Marko 16:15-18

Umisheni ndiyo moyo wa Mungu ndio kusudi kubwa la Mungu, kusudi maalumu ni kumuokoa mwanadamu, Na alilonena akiwa dunia alikuwa ananena kile alichopewa na Baba yake kuzungumza, Marko 16:15-18, haya ni maneno ya mwisho aliyowaachia wanafunzi wake wakati anakaribia kurudi Mbinguni, maeno haya ni ya msingi sana, ndio yanayokamilisha ujio wake wa kuja duniani. Hakuna anayeokolewa na kukaa tu ni lazima uwe na shughuli maalumu. Sisi kama watu tuliookolewa na Yesu tunawajibu ufwatao:

 1.KUMUWAKILISHA BWANA YESU HAPA DUNIA, Matendo 1:8, kumuwakilisha Jina lake maeneo ambayo hayajafikiwa 

2.KUWAFANYA WALIOOKOLEWA KUWA WANAFUNZI, yani waliookolewa kuwafundisha Neno la Mungu ili na wao wachukue jukumu lilelile la kuwashuhudia wengine habari za Yesu

3.KUWAJULISHA NGUVU YA UTENDAJI AMBAYO NDIO ROHO MATAKATIFU, Roho Mtakatifu ni nyenzo ya kupeleka injili 

4.KUWA MCHUNGAJI MWEMA, chunga uchungaji wako na wapeleka kondoo katika malisho mema

5. KUWAPELEKA WATENDA KAZI SHAMBANI, Warumi 10:15
 Ni jukumu letu kupeleka injili mahali mbalimbali yasiyofikiwa kwa kuchangia na kuwaombea Watu wali tayari kwenda maeneo hayo. Changizo kwa ajili ya umisheni hazijaanza leo Wafili 4:14-20, watahubirije wasipo pelekwa, swala la kuwapeleka halikuanza leo ni kanuni kabisa ambayo ipo kwenye biblia, Yeremia 47:7, hatuta kwenda wote lakini tutaenda kwa changizo zetu, Bwana Yesu anapenda kumuona mtu anayetoa kwa moyo wa ukunjufu na kwa moyo wa kupenda, wamishenari ni wajumbe, ni wawakilishi wa jina la Yesu hebu tuwabeleke wamishenari, na Bwana Yesu atajitokeza katika maisha yako hautapungukiwa tena.

No comments:

Post a Comment