''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, June 16, 2019

UHITAJI WA MACHO YA ROHONI

Mhuburi: Mch. Kiongozi Abdiel Mhini
Maandiko: 2Wafalme 6:8-23

Elisha alikuwa ana macho ya rohoni, alikuwa anajua mipango yote ya Mfalme wa Shamu hata kama akipanga akiwa chumbani kwake, Elisha aliyajua hayo kwasababu alikuwa na macho ya kiroho. 

Elisha alijua mipango ya shamu, ni kwasababu tu alikuwa na Roho Mtakatifu, alikuwa Rohoni. Unahitaji macho ya rohoni kuona vitu vya mbele yako, kuona vitu vya sirini. Kuwa na macho ya Roho kuna faida sana kwasababu utajua hila zote za shetani na mipango yake anayotaka kuitumia kukuangusha.

Tatizo kubwa la wakristo wengi wa sasa ni kutokuwa na muda mzuri wa kukaa na Mungu, kusoma Neno lake na kulitafakari kwa undani, kutumia muda katika kuomba. Ni lazima utengeneze uhusiano wako na Mungu uwe vizuri.

Mathayo 16:23 Yesu hapa aliweza kugundua kama Petro katumiwa na shetani kwasababu alikuwa Rohoni, na akaweza kumkemea kwasababu alikuwa ana nguvu za rohoni. Ili  kuvunja ngome za shetani ni lazima uwe na nguvu za rohoni. Kuna macho ya nyama na macho ya rohoni, jitahidi sana uwe na macho ya rohoni; hila za shetani huwa hazionekani hivi hivi mpaka uwe na macho ya kiroho.

Utapataje Macho ya Rohoni?
  1. Kwa Kusoma Neno la Mungu, bila Neno hutaweza, Ishi katika Roho. Ukiliamini Neno la Mungu linakufungua sana katika ulimwengu wa kiroho na unaanza kuona mambo zaidi.
  2. Kulitii Neno la Mungu, Yohana 9:35-41, unaweza ukalijua Neno lakini usilitii, kutii Neno ndiko kunako badilisha.
  3. Kumwamini Mungu kwa asilimia zote 100% Warumi 4:1-3 Huna macho ya kiroho Kwasababu humwamini Mungu asilimia zote na huamini Neno lake asilimia yote, Abraham alimwamini Mungu kwa asilimia zote, kumwamini Mungu asilimia yote ni kwa muhimu sana, KUNA MAMBO HUTAYAONA MPAKA UTAKAPO AMUA KUMWAMINI MUNGU KABISA KUAMINI ANACHO KWAMBIA, USIWE KIPOFU, JIACHILIE KWA MUNGU, USIWE MKRISTO VUGUVUGU

1 comment: