''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, February 24, 2013

UJUMBE WA LEO: KUMGUSA MUNGU KIBINAFSI
-------------------------------------------------------
MAANDIKO:  Marko 5:25-34, Luka 7:44-48
MHUBIRI: MRS. MASEMBO
-------------------------------------------------
Kumgusa Mungu ni kufanya kitu cha ziada kwa ajili ya Mungu, ndio umeokoka lakini je? Unafanya kitu kipi cha ziada kwa ajili ya Mungu?. Kuokoka peke yake hakutoshi  unatakiwa baada ya kuokoka ufanye kitu Fulani ambacho kitamgusa Mungu mojamoja.

Yule kahaba alimgusa Yesu kwa matendo yake, alimfuta Yesu kwa nywele zake alimbusu miguu yake na kumpaka Yesu marhamu. Ndio Yule Simoni alikaribisha Yesu lakini hakufanya zaidi ya hapo, Je? Leo umefanya kitu gani cha zaidi cha kumgusa  Yesu?.Tafuta leo ni kitu gani utakacho kifanya ili umguse Yesu. 

Yule mama aliyetokwa na damu miaka 12, aliamua kufanya kitu cha ziada kwa kugusa vazi la Yesu kwa imani naye akapokea uponyaji wake.  Aliamini kwamba hata akigusa tu vazi la Yesu atapona. Unatakiwa kumgusa Yesu KIBINAFSI, ndio unaunda kanisani lakini  Je? Umemgusa Mungu kibinafsi?

Kumbuka kwamba huyu mwanamke aliyetokwa na damu alikuwa haruhusiwi kuchangamana na watu lakini aliposikia Yesu mtenda miujiza amekuja hakujali kwamba ataonekana na mafarisayo lakini alikuwa tayari kwa chochote kile ilimradi amguse Yesu. Usijali watu watasema nini juu yako wewe jitahidi kufanya kitu ambacho kitamgusa Yesu.

Unaweza kumgusa Mungu kwa mali zako, au kwa nguvu zako kama kufanya kazi nyumbani mwa Bwana kupiga deki kanisa, ni lazima utafute chochote cha kufanya kwa Mungu ambacho kitamgusa Yeye. Ni jambo gani linalokutesa kwa muda mrefu sasa, ingia gharama ya kufanya kitu kitakacho mgusa Yesu.

Fanya uamuzi leo na chukua hatua kama huyo mama alivyosema, mwambie Mungu imetosha mimi kuendelea kukaa na shida hii halafu mguse kwa kufanya kitu na Mungu atakujibu shida yako. Pia kwa kumtafuta Mungu kwa bidii sana  Mithali 8:17. ‘inawezekana kubadilisha hali yoyote uliyonayo’

1 comment:

  1. For sure, hili neno nami limenigusa sana, Je katika kizazi hiki ni watu wangapi wanamgusa Mungu kwa matendo yao, je matendo yetu kama kanisa la Bwana tunamgusa Mungu? For sure hatuna budi kukaa na kujitafakari tena kwa upya kwamba Je? Tunamgusa Mungu au tupo tu kawaida, and nothing extra we do???

    ReplyDelete