''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, April 7, 2013

UJUMBE WA LEO: USHINDI JANGWANI (VICTORY IN THE WILDERNESS)
----------------------------------------------------------------------------------
MHUBIRI: PASTOR REV. EZEKIEL MWAKAJWANGA
MAANDIKO: Mathayo 4:1-11
 ---------------------------------------------------------
Tunaona Roho alimpeleka Yesu jangwani, hebu jiulize Kwanini Roho wa Mungu mwenye huruma na upendo alimpeleka Yesu jangwani?, wakati jangwani ni sehemu ya shida?.Tambua ya kuwa kuna uhusiano kati ya jangwa na ushindi, mtu wa Mungu huwa anapita kwenye vyote yaani kwenye jangwa na ushindi, na fahamu kwamba jangwa na ushindi vinaenda pamoja na jiandae kwa ushindi wako katika jangwa. Watakatifu wote waliofanikiwa katika Biblia walipita jangwani, mfano Yusufu ambaye mwishoni alikuwa mwenye cheo kikubwa sawa sawa na waziri mkuu lakini alipitia majaribu mengi kama kuuzwa na ndugu zake kuwa mtumwa alipitia kuwekwa jela, lakini kote huko hakumuacha Mungu hatimaye akashinda, ilimpasa apitie katika majaribu yale ili baadaye apate kile cheo. Pia Yesu kabla hajaanza huduma Roho alimpeleka jangwani maana huko ndo kwenye ushindi. Yesu alianza ushindi wake kule jangwani, kila mkristo ana jangwa lake lakini wale wanaovumilia mpaka mwisho wataokoka, Ufunuo 2:10. Usitamani njia ya mkato maana huko ndo kuna baraka  ambazo sio za kweli, pita njia iliyo sahihi ili upate mafanikio yatakayo mpa Mungu utukufu, Yakobo 1:2-4,12.

Kwahiyo ndugu yangu ili ufanikiwe sana ni LAZIMA ukubali kupita jangwani maana huko ndo kwenye ushindi wako, maana huko ndiko utakapojifunza kutembea vizuri na Mungu, kwahiyo furahia unapopita kwenye majaribu maana ukitoka huko huwi tena mtu wa kawaida.

Amua sasa kukubali kuingia jangwani lakini huku ukiwa na Roho Mtakatifu. Maana kuna majangwa/majaribu mengine yasiyotoka kwa Mungu bali unajisababishia mwenyewe mfano unapofanya dhambi mwenyewe au majaribu mengine ni mateso yanayosababishwa na shetani. Tambua ya kuwa katika kila mafanikio shetani atakuwepo kukujaribu.

shetani alimwambia Yesu kwamba ajitupe kwakuwa malaika watamchukua lakini Yesu kwa kujua Yeye ni nani na Mungu ni nani akamjibu shetani imeandikwa usimjaribu Bwana Mungu wako. Watu waliookoka wengi sasa kwa kutokujua wao ni Nanina Mungu wanaomwabudu ni nani hasa wanaachilia haki zao bila kujua. Ni kweli hilo andiko la malaika watakuchukua usije ukajikwaa lipo katika Zaburi 91:11 lakini halikusema utakapojitupa mwenyewe. Kuwa makini sana shetani huwa anatabia ya kutumia maneno ya Mungu wakati usiopasa ili kukujaribu. shetani alitaka kumpa Yesu ushindi kwa style anayotaka yeye, si  kila kitu au kila muujiza au kinachofanya kazi ni cha ki-Mungu. Mathayo 7:21-23.

Kuwa makini sana shetani ni mjanja, alimwonyesha Yesu milki yote akamwambia atampa vyote kama akimsujudia akawahau kwamba Yesu ndio aliyeviumba hivyo vitu na dunia nzima. Ndugu yangu mwabudu Mungu peke yake tu, hata kama unapitia katika mambo magumu kiasi gani usitafute njia ya mkato, kuwa mwaminifu unapokuwa jangwani.

Unapokuwa jangwani/katika majaribu kumbuka msaada upo karibu, unaweza ukaona kimya lakini kumbuka mwisho ndiko kuzuri vumilia, Yesu baada ya kumaliza majaribu Malaika walikuja kumtumikia, Yusufu baada ya lumaliza majaribu mwisho alikuwa waziri mkuu. Usikate tama mwisho ndo kuzuri.















No comments:

Post a Comment