''Badilisha Maisha yako kwa kumpokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wa Maisha Yako.''

Sunday, May 12, 2019

RIDHIKA NA ULICHONACHO

Mhubiri: Ndg Leandri Kinabo
Maandiko: Wafilipi 4:10-13

Wafilipi 4:10-13 "kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa waaminio. 11 Mambo hayo uyaagize na kuyafundisha. 12 Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi. 13 Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma na kuonya na kufundisha."

Kurithika wakati unapopitia majaribu ni kitendo cha imani, ni kitendo cha kumuamini  kwamba Mungu atakuwezesha. Paulo aliandika sura hiyo alipokuwa gerezani, unaweza kusema alikuwa katika jaribu/ mapito, lakini haikujalisha anapitia hali ngumu kiasi gani, yeye alizidi kumwamini Yesu na kurithika huku akijua kwamba Mungu atamuokoa.

Kutokuridhika huwa kunaanzia ndani ya moyo, unapokosa uhusiano mzuri na Mungu unaanza kuwa na mashaka unaona kama kuna uwezekano Mungu asifanye kitu kuhusu shida yako unayopitia, lakini unapoamua kumwamini Yesu asilimia 100 utakuwa huna hofu  yoyote.

Kuridhika katika Bwana ni tunda la kumwamini Mungu. Ukimwamini Mungu hata kama unapitia katika hali ngumu kiasi gani tambua kuwa Mungu anakupenda na Mungu atafanya kitu kwa ajili yako. 

No comments:

Post a Comment